Thursday, March 23, 2017

Barnaba Afunguka ukweli kuhusu kuachana na Mama watoto wake>>>Soma ndani

Barnaba
Barnaba amefunguka kuhusiana na mahusiano yake na mama Steve kwa sasa.
Wiki chache zilizopita muimbaji huyo alidaiwa kuachana na mzazi mwenzake huyo ambaye wamefanikiwa kupata mtoto mmoja.
Akiongea kwenye kipindi cha XXL cha Clouds FM, hitmaker huyo wa Lover Boy amesema, “Kwa sasa siko kwenye maelewano mazuri na mama watoto wangu. Sio kwamba tumeachana au tumetengana sitaki kusema hivyo.”
“Siwezi kusema simpendi mwanamke niliyepata nae mtoto [mama Steve],yule ameshakua kama ndugu yangu.Namrespect sana mama Steve ila kila mtu anaendelea na maisha yake na hatutaki kutengeneza picha mbaya kwa mwanetu,” ameongeza.
Wakati huo huo Barnaba amesisitiza kuwa wimbo wake mpya wa ‘Lonely’ ambao ameuachia leo haujamgusa mtu yoyote na wala hausiani na maisha yake.

CHANZO CHA HABARI NA:teamtz.com


Endelea kuitembelea DJ WILLKAN BLOG
kwa kulike Page yetu ya Facebook,..DJWillkan.com, pia Instagram: @djwillkan_zekanvol
tufollow pia Twitter: @Djkanvol
 

No comments:

Post a Comment