Sunday, July 20, 2014

JINSI MWANAMKE ALIVYOJIPATIA MAMILIONI KUTOKANA NA UVUTAJI WA SIGARA WA MUME WAKE


sigarr
Kampuni ya upili kwa ukubwa katika utengenezaji wa sigara nchini Marekani imeagizwa kulipa kitita kikubwa cha dola billioni 23 kwa mke wa mwathiriwa mmoja wa sigara aliyefariki kutokana na saratani ya mapafu.
Kwa mujibu wa shirika la habari la BBC, Mjane huyo Cynthia Robinson alichukua hatua dhidi ya kampuni ya sigara ya R.J Reynolds baada ya kifo cha mumewe aliyekuwa na miaka 36.
Kampuni hiyo imeyataja malipo hayo kama yasio na haki na kusema kuwa itakata rufaa.
Wakili wa bi Robinson amesema kuwa kampuni hiyo ya sigara iliuza sigara hizo bila kutoa tahadhari yoyote kuhusu tishio la uvutaji wake.


                                                Habari moto moto na djwillkan.com

No comments:

Post a Comment